Thursday, October 2, 2014

VITUKO VYA MASTAA ;AMBER ROSE NA WIZ KHALIFA


Amber1Kuvunjika kwa ndoa ya mastaa Amber Rose na Wiz Khalifa kumeendelea kuchukua nafasi kwenye headlines za dunia na hii ni baada ya Amber kutaja chanzo mojawapo cha kuvunjika kwa uhusiano huo.
Kwenye interview ya Radio Amber amesema kingine kilichomkasirisha ni kuona Wiz anawaendekeza warembo flani wawili mapacha ambao inaaminika amekua akijihusisha nao kimapenzi.
Amber amesema alipenda kuiokoa ndoa yake ili waendelee kuwa pamoja lakini anaeonekana kukataa kuendelea kuwa kwenye ndoa ni Wiz mwenyewe, Amber anasema hata taarifa za mwanzoni kwamba walitengana siku nyingi kabla ya kutaka talaka zilikua za uongo…. hakufanya maamuzi yao sababu alitaka kuiokoa ndoa yake. amber 2Amber amemshutumu Wiz kwa kutoka kimapenzi na hawa mapacha kwenye hii picha hapa chini…
amber 3

Wednesday, April 23, 2014

MWAIPAJA BLOG NDANI YA ULANGA

Mwanasheria Amani Mwaipaja akiwa Ndugu Mohamed Nguku ambaye ni Msaidizi wa kisheria kutoka kituo cha wasaidizi wa sheria Ulanga nje ya jengo la Chama cha Wasioona Ulanga. Mwanasheria Mwaipaja yuko wilayani Ulanga kwa ajili ya kutambulisha Mradi wa Kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa Huduma ya Msaada wa kisheria Mkoani Morogoro, mradi wa miaka miwili unaofadhiliwa na Legal Services Facility
Mwanasheria Amani Mwaipaja akiwa na Mtangazaji wa Radio Ulanga Fm Fatma Mtemangani nje ya ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Wadau wa Mradi wakisikiliza maelezo kutoka kwa mwanasheria Amani Mwaipaja (Hayupo pichani) ndani ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Ulanga
Nje ya ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
 Mto Kilombero kipindi cha Mvua unavyoonekana





Tuesday, April 22, 2014

MTANGAZAJI MADUHU ATEMBELEA STUDIO YA KWANZA RECORDS


Mtangazaji Mkongwe kwenye Tasnia ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano nchini Tanzania Maduhu Jumanne ( Mwenye Miwani) ambaye anafanya kazi kwenye kituo cha Radio cha Morningstar Radio na Televisheni ya Morningstar Tv inayomilikiwa na Kanisa la Waadventista Wasabato nchini Tanzania akiwa kwenye picha ya pamoja na Mtayarishaji wa Muziki wa Studio ya Kwanza Records ajulikanaye kwa jina la Vent Skillz
Mtayarishaji wa Muziki (Producer) wa Kwanza Records Vent Skillz akiwa kazini. Studio ya Kwanza Records inapatikana Morogoro Mjini ni studio maarufu na yenye mchango mkubwa katika kukuza, kuendeleza na kuibua vipaji na muziki wa Kitanzania

Saturday, October 5, 2013

J - MARTINS AWAPAGAWISHA MASHABIKI WA TANGA ,KATIKA TAMASHA LA FIESTA

pichani juu na chini ni Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria,J-Mrtin akitumbuiza jukwaani usiku wa leo,kwenye tamasha la Serengeti fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,ambaye pia ni mtoto wa Mkongwe wa muziki wa dansi hapa nchini,Mzee Zorro,Maunda Zorro akiimba kwa hisia jukwaani usiku huu kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga wakati tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea.
Mzee wa Masauti,Christian Bella akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu ndani ya uwanja wa Mkwakwani
Sehemu ya mashabiki wakishangweka huku manyunyu ya mvua yakisumbua hapa na pale usiku huu.span>
Mkali mwingine wa miondoko ya mitindo huru,God Zilla akishusha mistari yake mbele ya mashabiki wake waliokuwa wakiitikia kwa pamoja,ndani ya uwanja wa mkwakwani usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea,sambamba na hali ya hewa ya mvua mvua huku mashabiki wakiendelea kupiga mayowe na miluzi kila kona ya uwanja.
Mwanadada Linah ambaye anafanya vyema katika ya muziki wa Bongofleva akicheza na shabiki wake jukwaani.
Msanii ambaye ni muigizaji lakini pia anasumbua sana katika anga ya muziki wa bongofleva,Shilole sambamba na skwadi lake wakilishambulia vilivyo jukwaa usiku huu wakati tamasha la serengeto fiesta likiendelea ndani ya uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga. Picha zaidi nenda Jiachie Blog

Sunday, August 18, 2013

RWANDA KATIKA TASWIRA

Wabongo tuna kasafari karefu kidogo kwa upande wa Miundombinu, Vijana tusilale,bado mapambano

Friday, August 9, 2013

Alichokisema Lulu kuhusu ishu ya elimu na mastaa wa bongo


luluxShule ni kitu cha msingi sana kwa mtu yoyote hasa yule ambaye ni kioo cha jamii au kiongozi. Sasa muigizaji Lulu amechukua hatua zake kwenye hii ishu ya elimu pamoja na kusema maneno,”Gettin more knowledge…..!!!we have to learn….especially sisi celebrities wa bongo….wengi wetu tunaongeaga pumba sana in public…yan hatujui nini tuongee wapi!!!!juc an advice lakni…..!!!!AM GOOD TO GO….”

Thursday, July 4, 2013

NDEGE WA TATU (NDEGE 3) NI KUNDI JIPYA JIJINI DAR ES SALAAM

Kutoka kushoto ni Paulyne Zongo, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Joan Matovolwa.Wanamuziki hao watatu na wakongwe nchini ndio wanaounda kundi hilo litakalojulikana kwa jina la NDEGE 3
Kundi la Ndege 3 linaloundwa na wanamuziki wakongwe katika Tasnia ya muziki wa dansi na kizazi kipya Joan matovolwa, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Paulyne Zongo, hivi karibuni limeshatoa kibao chake kinachokwenda kwa jina la 'MISUKOSUKO YA MAPENZI' ambacho redio kadhaa nchini zimeanza kukirusha.
 
MISUKOSUKO YA MAPENZI ni nyimbo ambayo imetungwa kwa umahiri wa hali ya juu, na kuonyesha viwango vya juu katika uimbaji na utunzi.
 
Kwa sasa Joan Matovolwa na Paulyne Zongo ni wanamuziki huru wakati Khadija Mnoga (Kimobitel) ni mwanamuziki anayeimba katika bendi ya Extra Bongo inayoongozwa na Camarade Ally Choki.

Friday, June 14, 2013

PICHA ZA KALA JEREMIAH AKITOA TUZO YAKE YA HIP HOP KWA MAMA WA MANGWEA




Mama mzazi wa marehemu Albert Mangweha akiwa ameshikilia tuzo aliyopewa kwa niaba ya mwanae, tuzo hii aliipata msanii Kala Jeremiah kwenye tuzo za Kilimanjaro ikiwa kama tuzo ya msanii bora ya Hip Hop 2013-14

TASWIRA NDANI YA BLOG


Thursday, June 13, 2013

MSAANI WA BONGO FLEVA AITWAYE LANGA AFARIKI DUNIA


ASHA BOKO KUTOKA KIVINGINE

Msanii Mkongwe wa Luninga na Vichekesho nchini Tanzania Asha Boko anategemea kuachia Video yake ya Kibonge Mnene mwisho wa mwezi huu. Video hiyo ambayo Audio yake ilifanyika katika Studio ya Kwanza Records iliyopo Morogoro imetayarishwa na Fasdo Video.Kwanza Records ni moja ya studio bora nchini Tanzania ambayo imekuwa ikisaidia kuinua vipaji vy muziki wa Bongo Fleva. Kwa wale wanaokumbuka Kwanza Records kwa mara ya Kwanza iliweza kumtambulisha Msanii Kitale aliyomshirikisha Marehemu Sharo Milionea iitwayo Hili Dude Noma.

Akiongea na Timu ya Mwaipaja Blog, Asha Boko amesema kuwa wadau wa Muziki wa Bongo Fleva wakae mkao wa kula kwakuwa amefanya mambo makubwa ndani ya Video hiyo.Asha Boko ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kufanya naye kazi ikiwemo filamu, movie na Bongo Fleva.

Kwa watakaohitaji kuwasiliana na Asha Boko wawasiliane nae kwa namba yake ya mkononi ambayo ni 0754 273904 ila wasibip wala kumwomba Vocha

ASHA BOKO KUACHIA VIDEO YAKE MWISHO WA MWEZI

Msanii Mkongwe wa Luninga na Vichekesho nchini Tanzania Asha Boko anategemea kuachia Video yake ya Kibonge Mnene mwisho wa mwezi huu. Video hiyo ambayo Audio yake ilifanyika katika Studio ya Kwanza Records iliyopo Morogoro imetayarishwa na Fasdo Video.Kwanza Records ni moja ya studio bora nchini Tanzania ambayo imekuwa ikisaidia kuinua vipaji vy muziki wa Bongo Fleva. Kwa wale wanaokumbuka Kwanza Records kwa mara ya Kwanza iliweza kumtambulisha Msanii Kitale aliyomshirikisha Marehemu Sharo Milionea iitwayo Hili Dude Noma.

Akiongea na Timu ya Mwaipaja Blog, Asha Boko amesema kuwa wadau wa Muziki wa Bongo Fleva wakae mkao wa kula kwakuwa amefanya mambo makubwa ndani ya Video hiyo.Asha Boko ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kufanya naye kazi ikiwemo filamu, movie na Bongo Fleva.

Kwa watakaohitaji kuwasiliana na Asha Boko wawasiliane nae kwa namba yake ya mkononi ambayo ni 0754 273904 ila wasibip wala kumwomba Vocha

Wednesday, June 5, 2013

MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEHA WAAGWA LEADERS (DAR) NA KUSAFIRISHWA KWENDA MOROGORO KWA MAZISHI.


 Msemaji wa Kamati ya Mazishi ya Marehemu Albert Mangwea ambaye pia ni Director kutoka Visual lab Bw Adam Juma akielezea ratiba ya Shughuli nzima ya Mazishi itakavyokuwa mara baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho zitakapomalizika
 Baadhi ya Wasanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Wa Kwanza Kabisa ni Mkoloni akifuatiwa na Madee ambaye ni wa Tatu kutoka Mbele wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Marehemu Albert Mangwea
 Msanii Wa Muziki wa Kizazi Kipya Nasibu Abdul almaarufu kama Diamond akipita kutoa heshima zake za mwisho.
Baadhi ya Wasanii wa Fani mbalimbali pamoja na ndugu,jamaa na marafiki wakipita pembezoni mwa jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Albert Mangwea na kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu Albert Mangwea leo katika viwanja vya leaders
 Msanii wa Muziki Keisha (aliyejifunga kiremba Cheupe) akifuatiwa na Noora wakiwa na nyuso za huzuni wakati wakipita kwaajili ya kutoa heshima zao za mwisho katika viwanja vya leaders
 Wasanii wa fani ya Maigizo hapa Nchini Mzee Magari (aliyeshika Koti jeusi) akifuatiwa na Msanii Natasha Pamoja na Monalisa wakipita kwaajili ya Kutoa Heshima zao Za mwisho kwa Marehemu Albert Mangweha leo katika Viwanja vya leaders
Baadhi ya Ndugu, Jamaa na Marafiki wakitoa Heshima za Mwisho
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu  Albert Mangweha likiwa juu ya meza tayari kwa Wakazi wa Jiji la Dar Kuanza kutoa Heshima Zao za Mwisho katika Viwanja Vya Leaders.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Habari, utamaduni na Michezo Bi Lilian Bereko akitoa Salamu za Rambirambi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo leo katika viwanja vya leaders kabla ya Wakazi wa Jiji la Dar hawajaanza kutoa heshima zao za mwisho
Mmoja kati ya watu wa karibu wa Marehemu Albert Mangwea ambaye pia ni msanii wa muziki wa Kizazi kipya kutoka Katika Kundi aliloanzisha Marehemu Albert Mangwea Mez B akitoa historia fupi ya Kundi la Chamber Squade katika viwanja  vya leaders. Picha zote kwa hisani ya Lukaza Blog

Sunday, June 2, 2013

New video (Coming soon!)

Hii ndo habari ya mjini,kaa mkao wa kuburudika kutazama video mpaya ya Ashaboko akiwa na Mycoely pamoja na Stan Bakora,Ngoma inaitwa Kibonge mnene,imetengenezwa studio za Kwanza Records chini ya producer Vennt Skillz.

Wednesday, May 22, 2013

BRAND NEW VIDEO: BRACKET- TEMPERATURE

One of Nigerians favorite duos Bracket is back with their long awaited video – Temperature brought to you by Ape Planet, a Capital Dream pictures production.