Thursday, July 4, 2013

NDEGE WA TATU (NDEGE 3) NI KUNDI JIPYA JIJINI DAR ES SALAAM

Kutoka kushoto ni Paulyne Zongo, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Joan Matovolwa.Wanamuziki hao watatu na wakongwe nchini ndio wanaounda kundi hilo litakalojulikana kwa jina la NDEGE 3
Kundi la Ndege 3 linaloundwa na wanamuziki wakongwe katika Tasnia ya muziki wa dansi na kizazi kipya Joan matovolwa, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Paulyne Zongo, hivi karibuni limeshatoa kibao chake kinachokwenda kwa jina la 'MISUKOSUKO YA MAPENZI' ambacho redio kadhaa nchini zimeanza kukirusha.
 
MISUKOSUKO YA MAPENZI ni nyimbo ambayo imetungwa kwa umahiri wa hali ya juu, na kuonyesha viwango vya juu katika uimbaji na utunzi.
 
Kwa sasa Joan Matovolwa na Paulyne Zongo ni wanamuziki huru wakati Khadija Mnoga (Kimobitel) ni mwanamuziki anayeimba katika bendi ya Extra Bongo inayoongozwa na Camarade Ally Choki.

Friday, June 14, 2013

PICHA ZA KALA JEREMIAH AKITOA TUZO YAKE YA HIP HOP KWA MAMA WA MANGWEA




Mama mzazi wa marehemu Albert Mangweha akiwa ameshikilia tuzo aliyopewa kwa niaba ya mwanae, tuzo hii aliipata msanii Kala Jeremiah kwenye tuzo za Kilimanjaro ikiwa kama tuzo ya msanii bora ya Hip Hop 2013-14

TASWIRA NDANI YA BLOG


Thursday, June 13, 2013

MSAANI WA BONGO FLEVA AITWAYE LANGA AFARIKI DUNIA


ASHA BOKO KUTOKA KIVINGINE

Msanii Mkongwe wa Luninga na Vichekesho nchini Tanzania Asha Boko anategemea kuachia Video yake ya Kibonge Mnene mwisho wa mwezi huu. Video hiyo ambayo Audio yake ilifanyika katika Studio ya Kwanza Records iliyopo Morogoro imetayarishwa na Fasdo Video.Kwanza Records ni moja ya studio bora nchini Tanzania ambayo imekuwa ikisaidia kuinua vipaji vy muziki wa Bongo Fleva. Kwa wale wanaokumbuka Kwanza Records kwa mara ya Kwanza iliweza kumtambulisha Msanii Kitale aliyomshirikisha Marehemu Sharo Milionea iitwayo Hili Dude Noma.

Akiongea na Timu ya Mwaipaja Blog, Asha Boko amesema kuwa wadau wa Muziki wa Bongo Fleva wakae mkao wa kula kwakuwa amefanya mambo makubwa ndani ya Video hiyo.Asha Boko ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kufanya naye kazi ikiwemo filamu, movie na Bongo Fleva.

Kwa watakaohitaji kuwasiliana na Asha Boko wawasiliane nae kwa namba yake ya mkononi ambayo ni 0754 273904 ila wasibip wala kumwomba Vocha

ASHA BOKO KUACHIA VIDEO YAKE MWISHO WA MWEZI

Msanii Mkongwe wa Luninga na Vichekesho nchini Tanzania Asha Boko anategemea kuachia Video yake ya Kibonge Mnene mwisho wa mwezi huu. Video hiyo ambayo Audio yake ilifanyika katika Studio ya Kwanza Records iliyopo Morogoro imetayarishwa na Fasdo Video.Kwanza Records ni moja ya studio bora nchini Tanzania ambayo imekuwa ikisaidia kuinua vipaji vy muziki wa Bongo Fleva. Kwa wale wanaokumbuka Kwanza Records kwa mara ya Kwanza iliweza kumtambulisha Msanii Kitale aliyomshirikisha Marehemu Sharo Milionea iitwayo Hili Dude Noma.

Akiongea na Timu ya Mwaipaja Blog, Asha Boko amesema kuwa wadau wa Muziki wa Bongo Fleva wakae mkao wa kula kwakuwa amefanya mambo makubwa ndani ya Video hiyo.Asha Boko ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kufanya naye kazi ikiwemo filamu, movie na Bongo Fleva.

Kwa watakaohitaji kuwasiliana na Asha Boko wawasiliane nae kwa namba yake ya mkononi ambayo ni 0754 273904 ila wasibip wala kumwomba Vocha